4 w - Translate

Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza katika Mahafali ya 24 ya Chuo Kikuu cha Abdulrahman Al Sumait Chukwani Wilaya ya Magahribi B, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 25 Januari 2025

4 w - Translate

RAIS MWINYI:VYUO VIKUU VIJIKITE KATIKA TAFITI ZENYE TIJA KWA JAMII.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amevikumbusha Vyuo Vikuu Viliyopo nchini Umuhimu wa kujikita katika Kufanya Tafiti ambazo zitatoa Ufumbuzi wa Changamoto za Kijamii na kuzisambaza kwa Watumiaji.

Rais Dk.Mwinyi ameyasema hayo katika Mahafali ya 24 ya Chuo Kikuu cha Abdulrahman Al Sumait Chukwani Wilaya ya Magahribi B, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Aidha, Rais Dk.Mwinyi ametoa Wito kwa Viongozi wa Vyuo Vikuu kuendelea Kujenga Uwezo wa kufanya Tafiti kwa Wafanyakazi kwa kutumia Fursa ziliyopo pamoja na Kushirikiana na Vyuo Vikuu vya vyengine vyenye Wataalamu Waliobobea katika Tafiti kwa ajili ya kuwajengea Uwezo Wataalamu Wazalendo.

Halikadhalika Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa ni Muhimu kwa Wizara na Idara za Serikali kushirikiana na Vyuo Vikuu kufanya Tafiti na kutumia Tafiti mbalimbali kuleta Maendeleo katika Nyanja za kijamii,Kiuchumi na Kiutamaduni.

Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali inathamini juhudi za Chuo Kikuu cha Abdulrahnan Al Sumait katika Utoaji wa Elimu kwani kunachangia Nguvu kazi na Ongezeko la Waatalamu Wazalendo katika Sekta Mbalimbali za Umma na Kijamii.

Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi ameahidi Serikali Kuendelea kutoa Ushirikiano wa kiwango cha juu ili Chuo hicho Kifikie malengo ya Kuanzishwa kwake.

Wahitimu 304 katika fani mbalimbali wamehitimu Katika Mwaka wa Masomo 2023-2024 ,Wanawake wakiwa 203 na 101 Wanaume, na kufikisha Wahitimu 4,993 waliohitimu katika Chuo hicho tangu Kuanzishwa kwake Mwaka 1998.

image
image
image
image
image
5 w - Translate

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi ameshiriki Mkutano Mkuu Maalum wa CCM , uliofungwa rasmi na Mwenyekiti wa CCM Taifa , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt.Samia Suluhu Hassan leo tarehe 19 Januari 2025 katika Ukumbi wa Mkutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Aidha, Dk.Mwinyi amethibitishwa na Mkutano huo Mkuu Maalum kuwa Mgombea wa Urais pekee wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi mkuu mwaka huu.

Vilevile, Mkutano huo umemchagua Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Mgombea pekee wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM na Dk.Emmanuel John Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza.

image
image
image
image
5 w - Translate

Actwazalendo
"Takwa la wananchi walio wengi Zanzibar hawataki kura ya siku 2 walilieleza 2020 hawakusilizwa na watu 21 wakauwawa sasa wanasema tena na sisi tunasimamia maamuzi yao juu ya jambo hili na tupo tayari kufa"

Source: ACT-Wazalendo Zanzibar

#tanzaniacommunitynetwork
#act-Wazalendo-Zanzibar

5 w - Translate

Ccm
Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar , Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, akishiriki Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Taifa unaofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 18 Januari , 2025.

Mkutano huo umefunguliwa leo na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan.

#ccmtanzania

About

Pata Habari kwa njia ya mtandao kupitia simu yako au computer yako ukiwa na Tanzania Community buree kabisa